KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Kati, inamshukuru Mungu kwamba katika hekima yake isiyopimika, na kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo, ametuunganisha waumini wake wote ulimwenguni kuwa wamoja.

Kwa njia hiyo, tunaweza kushirikiana pamoja na kufanikishwa katika mambo mengi. Dayosisi yetu inajihusisha na huduma mbalimbali za kijamii, kiroho, kiuchumi na kiakili kupitia idara za Misioni na Uinjilisti, Jinsia, Diakonia, Ibada na Muziki, Afya, Elimu, Mipango, Fedha na Utawala. Dayosisi ina Majimbo Saba Kanisa Kuu na Sharika 137.

Tovuti hii kwa namna iliyo bora, inaeleza mambo yote yanayofanywa na Dayosisi hii pamoja na Uongozi wake. Tunakukaribisha kutembelea Tovuti yetu.

“Tazama jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja”. Zab 133:1.

Wenu,

Askofu Dkt. Godson Abel Mollel

Mkuu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Kati.

KUHUSU SISI

Dayosisiya Kaskazini kati ya KKKT ilianza mwaka 1973, wakati huo ikijulikana kwa jina la Sinodi Mkoani Arusha, iliyoongozwa na Mchungaji Mesiaki Kilevo; akiwa kiongozi wa kwanza wa Sinodi ikiwa na Washarika 30,000, Sharika 20 na Mitaa 110.

Kiongozi wa Pili wa Sinodi alikuwa hayati Askofu Dkt Thomas Olmorijoi Laiser kuanzia mwaka 1980 hadi mwaka 1986.

Mwaka huo wa 1986 Sinodi ilibadilika kuwa Dayosisi Mkoani Arusha na Askofu wa kwanza akawa hayati Askofu Dkt Thomas Olmorijoi Laiser.

Mwaka 2010 Dayosisi Mkoani Arusha ilibadili jina na kuwa Dayosisi ya Kaskazini Kati, baada ya Serikali ya awamu ya tatu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kuamua kuugawa Mkoa wa Arusha na kutokeza mikoa ya Arusha na Manyara.

idara za dayosisi

Idara Ya Elimu

Inashughulika na usimamizi wa shule, maendeleo ya walimu, mitaala ya Kikristo, na kuboresha kiwango cha elimu katika dayosisi.

Idaya Ya Afya

Husimamia vituo vya afya vya dayosisi, kampeni za afya ya jamii, na kushirikiana na taasisi za afya kutoa huduma bora kwa jamii.

Idara ya Miradi na Mali

Inaratibu miradi ya maendeleo na uwekezaji wa mali za dayosisi kwa ajili ya kuongeza mapato na uendelevu wa huduma.

Idara Ya Hazina

Inahakikisha usimamizi bora wa fedha, uandaaji wa bajeti, ukusanyaji wa mapato, na utoaji wa taarifa za kifedha kwa uwazi.

Menejimenti ya Dayosisi

Dkt. Godson Abel
Mollel

Askofu

Mchg. Lareton Loishiye Lukumay

Msaidizi wa Askofu

Mwl. Solomon Loshilu Sambweti

Katibu
Mkuu

Mchg. Julius Rafael
Tarakwa

Naibu Katibu Mkuu-Misioni na Uinjilisti

CPA. Mussa Abraham Massanga

Naibu Katibu Mkuu-Mipango, Fedha na Utawala.